Hatima ya maisha ya Waafrika katika Bunilizi za Kiswahili: Mwegamo wa kifalsafa

No Thumbnail Available
Date
2021
Journal Title
Journal ISSN
Volume Title
Publisher
Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS)
Abstract
Makala hii imefafanua sababu za hatima ya maisha ya mwanadamu kulingana na fikra za Waafrika kwa kurejelea riwaya za Utengano (1980) na Tata za Asumini (1990). Data za msingi zilizofafanuliwa katika makala hii zimepatikana maktabani kwa kutumia mbinu ya usomaji makini. Nadharia ya Udhanaishi imetumika kama mwegamo muhimu katika uchambuzi na mjadala wa data zilizowasilishwa katika katika utafiti uliofanyika. Matokeo yanaonesha kuwa utajiri wa maarifa yaliyomo ndani riwaya teule husawiri maudhui na fikra halisi za Waafrika kulingana na tamaduni zao. Fikra hizo hudhihirisha falsafa inayotawala maisha yao. Pia, hubainisha sababu mbalimbali za hatima ya mwanadamu kulingana na mitazamo ya Waafrika. Kifo ni miongoni mwa sababu zilizobainika wazi katika riwaya teule kuwa kinasababishwa na maamuzi ya Mungu, maovu ya mwanadamu mwenyewe na watu wanaomzunguka katika mazingira yake halisi; na namna Waafrika wanavyofikiri juu ya sababu za hatima ya maisha yao. Mwandishi anayaonesha haya ili kudhihirisha uhalisi wa fikra za jamii yake kama sampuli ya jamii za Kiafrika. Makala hii inahitimisha kuwa fasihi andishi inahifadhi na kuonesha maarifa yanayoisawiri jamii husika.
Description
Paper submitted to the Ruaha Journal of Arts and Social Sciences (RUJASS)
Keywords
Falsafa, Fasihi, Hatima, Kifo na Mitazamo ya Waafrika, Bunilizi za Kiswahili, Mwegamo wa Kifalsafa, Hatima ya Maisha kwaWaafrika
Citation
APA
Collections