Communities & Collections
All of MUIR
  • English
  • العربية
  • বাংলা
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Ελληνικά
  • Español
  • Suomi
  • Français
  • Gàidhlig
  • हिंदी
  • Magyar
  • Italiano
  • Қазақ
  • Latviešu
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Srpski (lat)
  • Српски
  • Svenska
  • Türkçe
  • Yкраї́нська
  • Tiếng Việt
Log In
New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Fuluge, Adria"

Filter results by typing the first few letters
Now showing 1 - 1 of 1
  • Results Per Page
  • Sort Options
  • Thumbnail Image
    Item
    Tija za tohara kwa jamii za Kiafrika: Uchunguzi wa mhusika Omolo katika riwaya ya ua la faraja (2004)
    (Journal of Kiswahili and Other African Languages, 2025) Fuluge, Adria; Duwe, Martina
    Katika jamii nyingi za Kiafrika, tohara ni mchakato wenye thamani na tija kubwa kwa baadhi ya makabila, husuani kwa kijana wa kiume. Katika makabila hayo, asiyetahiriwa huonekana kuwa bado ni mtoto na hajakomaa kifikra na kiutu, ambapo huweza hata kutengwa katika kushirikishwa baadhi ya masuala ya kijamii. Kijana huyo kama umri wake ni mkubwa, huweza kudharauliwa na rika lake na hata waliopo chini yake. Sambamba na hilo, katika maisha halisi ya Waafrika, tohara huchukuliwa kwa thamani inayoweza kuendeleza na kuhifadhi utambulisho wa kitamaduni na kijamii. Kwao, tohara humfanya mtu atambulike kwa namna tofauti na ilivyokuwa awali. Kwa jumla, thamani ya tohara kwa Waafrika ni suala lililowashughulisha wataalamu wengi. Hata hivyo, pamoja na kuwepo kwa tafiti nyingi kuhusu tohara kwa Waafrika, bado tija za tohara kwa kufungamanisha na fasihi andishi haijamakinikiwa kwa umahususi wake. Kwa hiyo, makala hii inashughulikia jambo hilo kwa kumrejelea mhusika Omolo kutoka riwaya ya Ua la Faraja (2004). Data za matokeo haya zilipatikana maktabani kwa kutumia mbinu ya usomaji matini. Vilevile, misingi ya Nadharia ya Sosholojia ya Kifasihi imetumika katika mchakato wa kuchunguza, kuchanganua, na kuwasilisha data zilizozaa matokeo hayo. Mjadala unaonesha kwamba tohara katika maisha ya Waafrika ina tija mbalimbali kulingana na utoshelevu wa kaida zao. Makala hii inajadili tija nne; nazo ni: Kudumisha mila, kuleta heshima kwa mhusika, kujikinga na magonjwa, na kujenga ujasiri na ukakamavu.

MUIR software copyright © 2002-2026 LYRASIS

  • Privacy policy
  • End User Agreement
  • Send Feedback
Repository logo COAR Notify